Tuesday, December 27, 2011

Wizara ya Iraq yashambuliwa

Wizara ya Iraq yashambuliwa

 27 Disemba, 2011
Watu kama saba wameuwawa katika shambulio la bomu dhidi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ya Iraq, mjini Baghdad.
Mripuko mjini Baghdad juma lilopita
Wakuu wanasema kuwa mabomu hayo yalirpiuliwa ndani ya gari na mtu aliyejitolea mhanga nje ya wizara.
Mripuko huo unafuatia miripuko mikubwa ya Alhamisi ambapo watu kama 70 walikufa.
Ghasia hizo zimezidisha mvutano wa kisiasa na kidini ambao umetokeza tena baada majeshi ya Marekani kuondoka mwezi huu.
Makamo wa rais wa Marekani, Joe Biden amewaelezea viongozi wa Iraq, kwamba anatiwa wasi-wasi na ghasia hizo.

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...