Siku nzima ya jana madktari wa hospitali kuu ya taifa ya muhimbili wamekuwa wakikesha kuhakikisha wanainusuru roho ya kiongozi wao dkt ulimboka steven aliyetekwa na kupigwa.
madaktari hawa walihakikisha wanafanya kila waliwezalo kulifanya ili kufanikisha anapona.
mpaka alfajiri ya kumkia leo , madaktari hao wamekuwa wakisikika wakisema hali ya ulimboka bado sio nzuri lakini wanahakika atapata nafuu.
MADAKTARI MBEYA WATANGAZA VITA.
KITENDO cha kutekwa na kupigwa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari
Tanzania, Dk Stephen Ulimboka, kumeibua hisia kali kwa madaktari waliopo
katika Hospitali ya Rufaa Mbeya, huku wakisema kuwa Serikali haiwezi
kukwepa kuhusiana na kitendo hicho.
Wakizungumza na Mwananchi,
madaktari waliogoma hospitalini hapo huku wakikataa kabisa kuandikwa
majina yao walisema, watanzania wanatakiwa kutambua wazi kwamba Serikali
imetangaza vita na madaktari hao na kwamba wameitaka Serikali kutolea
ufafanuzi yakinifu kuhusiana na kupigwa kwa kiongozi huo.
Walisema
kitendo cha kutekwa kwa Dk Ulimboka, kamwe hawapo tayari kurudi kazini
licha ya kuwa baadhi yao walikuwa tayari kurejea kazini lakini kutokana
na hilo hawawezi kumsaliti Ulimboka kwa kitendo alichofanyiwa, na kudai
kuwa ndio kwanza mgomo huo umeanza rasmi sasa uliopita haukuwa mgomo.
“Kamwe
sisi hatupo tayari kurudi kazini tena, kwanza ndio mgomo umeanza rasmi
na kutokana na hali hii watanzania watambue wazi kwamba serikali
imechoka, tumetoka vijijini tutarudi kulima, lakini hatutamsaliti
Ulimboka” alisema mmoja wa madaktari hao huku akitokwa machozi.
Daktari
huyo ambaye yupo katika mafunzo ya vitendo alisema kuwa kumpoteza Dk
Ulimboka siyo mwisho wa kudai haki kwa kuwa ulimboka ni kiongozi tu na
suala la kudai maslahi yao yapo mikononi mwao hivyo wataendelea na
harakati zao hadi kitakapo eleweka.
“Kumwagika kwa damu ya Ulimboka
kumetengeneza akina Ulimboka wengi na damu yake italipwa na sisi kwa
kutomsaliti kwa namna yoyote ile na hiyo damu ya mpigaji mwenzetu ndio
kwanza imefumbua makucha yetu kuanzia sasa” alisema daktari huyo.
Hata
hivyo, Daktari bingwa ambaye pia hakutaka jina lake liandikwe alisema,
kitendo cha kutekwa kwa Dk Ulimboka hata wao ambao hawakuwapo katika
mgomo huo sasa, wanaingia kwenye mgomo huo rasmi kwa kile alichodai kuwa
ulimboka ni daktari kama wao.
No comments:
Post a Comment