Wednesday, June 27, 2012

URAIS 2015: ZITTO KABWE,Dkt. SLAA MCHUANO MKALI

    mbunge wa kigoma kaskazini, naibu kiongozi wa kambi ya upinzania bungeni na  naibu katibu mkuu wa CHADEMA-bara Mh;zitto kabwe akisalimiana na katibu mkuu wa chama hicho ambaye pia alikuwa mgombea wa urais katika uchaguzi mkuu uliopita Dkt.Wilbroad Slaa. mpaka sasa upigaji wa kura unaendelea katika blog hii na zitto kabwe anaonyesha kufanya vizuri baada ya kkujikusanyia kura 103 mpaka ninapoandika habari hii ambazo ni sawa na 42% huku dkt slaa yeye akiwa amejikusanyia kura 86 sawa na 35% ya kura zote zilizopigwa. hivyo basi wafuasi wa slaa wanakazi ya kufanya kama wanataka mgombea wao aonyeshe uimara wake kama aliouonyesha katika uchaguzi mkuu uliopita, hawana budi kumpigia kura kwa wingi.

     waziri wa ujenzi na miundombinu Dkt john magufuli ambaye pia ni mbunge wa chati-CCM akisisitiza jambo katika moja ya mikutano yake na vyombo vya habari. katika upigaji kura unaoendelea kwenye blog hii magufuli anashika nafasi ya tatu mbele ya mbowe kwa kuwa na ailimia 4 ya kura zote baada ya kujikusanyia kura kumi mpaka sasa.
                 pichani mwenyekiti wa taifa wa CHADEMA na kiongozi wa upinzani bungeni ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Hai mh; freeman mbowe ambaye yeye katika hatua hizi za mwanzo ameweza kujinyakulia kura tisa tu sawa na asilimia 3 nyuma ya magufuli mwenye asilimia nne. nayeye pia bado hajapoteza matumaini ikiwa wafuasi na wapenzi wake wana matumaini ya kumuweka kileleni ili awe wa kwanza hawana budi kumpigia kura kwa wingi.
   Dkt. Salim Ahmed Salim. katibu mkuu wa zamani wa umoja wa Africa na waziri mkuu mstaafu wa serikali ya jamuhuri ya muungano wa tanzania. yeye kwenye mchuano huu anafungana na spika mstaafu wa bunge la jamuhuri ya muungano wa tanzania ambaye pia ni mbunge wa urambo mashariki na waziri wa masuala ya afrika mashariki  mh;samweli sitta wote wanafungana kwa kuwa na asilimia 2 baada ya kila mmoja kujinyakulia kura saba.
  • Zitto anaongoza kwa kuwa na 42% ya kura zote zilizopigwa mpaka sasa
  • slaa anamfuatia kwa kuea na 35% mpaka sasa
  • magufuli naye achomoza kwa 4%
  • mbowe bado ana 3% ya kura zote
  • samwel sitta na dkt salim kila mmoja ana 2%
  • NI KATIKA UKUSANYAJI WA MAONI UNAOENDESHWA NA BLOG HII.   
upigaji wa kura katika shindano hili utaendelea katika blog hii kama inavyoonyesha kwenye upande wa kulia wa blog ambapo kura zitapigwa mpaka mkesha wa mwaka mpya kuingia 2013.
blog ya wajamaa inawatakia kila la heri wapenzi, washabiki na wafuasi wa wanasiasa hawa wanaochuanishwa katika kufanikisha wapendwa wao wanashinda.
blog yetu inaamini kuwa rais mzuri hapatikani kwa kampeni za siku 74 bali hupatikana mapema kwa kuonyesha matendo mema na uwezo unaoweza kumsimamia mbele ya jamii na kuonekana ana faa.

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...