Wednesday, June 27, 2012

UZAZI WA MPANGO AFRICA

Raia wa Nigeria wahimizwa kupanga uzazi

Wanawake wa Nigeria Sokoni

Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan anasema wakati umefika raia wake kupanga uzazi. Kiongozi huyo amesema kuna watoto wengi sana wanaozaliwa na ipo haja kuwepo na sheria ya kuwa na mpango wa uzazi.
Ameongeza watu wasio jua kusoma wala kuandika wameendelea kuwapata watoto wengi ambao wanashindwa kuwapa mahitaji muhimu ya maisha.Umoja wa Mataifa unakadiria idadi ya Nigeria kuongezeka kutoka milioni 160 hadi milioni 400 ifikapo mwaka 2050.
Nigeria inaongoza kwa idadi kubwa zaidi ya watu Afrika na juhudi za awali kuwashawishi wazazi kuwapata watoto wachache ziligonga mwamba.
Mwandishi wa BBC Will Ross amesema ongezeko la watu linapunguza raslimali hali inayotishia kuwepo na machafuko ya kushindania raslimali hususan arthi.
Rais Jonathan amesema ipo haja kuwepo na sheria ya kudhibiti idadi ya watoto wazazi wanaopata katika siku za usoni.
Amelitaka Baraza la Idadi ya watu kuanza kampeini ya kushawishi jamii umuhimu wa mpango wa uzazi.
Amesema japo suala hili ni nzito kutokana na misimamo ya kidini na kimila, ipo haja jamii kubadilisha mawazo kwamba watoto ni baraka kutoka kwa Mungu.
bbc

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...