Kisimayo yaundiwa mkakati
wakuu wa jeshi wa nchi hizo wanasema watafanya mikutano kadhaa kabla ya kutekeleza majukumu ya kijeshi.
Picha AP
Wakuu wa majeshi wa nchi za Afrika Mashariki na Sierra Leone
wanakutana mjini Nairobi Kenya kujadili jinsi ya kuiteka bandari muhimu
ya mji wa Kisimayo nchini Somalia inayodhibitiwa na wanamgambo wa Al
Shabab.
Mkutano huu unashirikisha nchi zenye wanajeshi katika jeshi maalumu
la muungano wa Afrika, Amisom lenye jukumu la kurejesha amani nchini
Somali.
Ingawa hakuna taarifa yoyote iliyotolewa kuhusu kuvamia mji wa
Kisimayo habari kutoka Nairobi zinasema wakuu hao wa majeshi watafanya
mikutano kadhaa kabla ya kutekeleza jukumu lolote la kijeshi.
Mkutano huu unafanyika wakati umoja wa mataifa umetoa onyo la kuonya
nchi za Afrika kuhusu mpango wa kufanya mashambulizi katika nchi za
Afrika hasa Kenya utakaotekelezwa na kundi hili la Al- Shabab.
VOA
No comments:
Post a Comment