Sunday, December 23, 2012

KIMENUKA KENYA

Baragoi Kenya wavamiwa na kuporwa mifugo Habari kutoka Kenya zinasema watu wanaotuhumiwa kuwa majambazi wamevamia kijiji kimoja karibu na mji wa Baragoi, kaskazini magharibi mwa Kenya na kuiba mamia ya mifugo. Majambazi hao karibu mia mbili wanasemekena kuwa na silaha nzito. Watu wengi wameripotiwa kuhama eneo hilo. Zaidi ya polisi arobaini waliuawa na wezi wa mifugo katika eneo hilo la Baragoi mwezi Novemba mwaka huu. Bunge la Kenya, Ijumaa liliitaka serikali kuunda Tume ya uchunguzi kuhusu kuuawa kwa polisi, tukio baya kabisa kuwahi kutokea katika historia ya nchi.

No comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...