Rais Wade wa Senegal akiri kushindwa
Matokeo yasio rasmi yanayo tangazwa na vyombo vya habari yanonesha Bw Sall anaongoza kwa wingi mkubwa dhidi ya Bw Wade
Picha AFP
"Huu ni mshangao mkubwa kwetu lakini tunafurahia kwamba wade amempigia simu Sall kumpongeza ni ushindi mkubwa kwa demokrasia.” asema Bi. Sow.
Matokeo rasmi hayatazamiwi hadi baadae wiki hii. Maelfu na maelfu ya wa Senegal walishirika Jumapili katika duru ya pili ya uchaguzi ulokua na ushindani mkali kati ya kiongozi mwenye umri wa miaka 85 na waziri mkuu wake wa zamani alyekua anaungwa mkono na viongozi wengine 12 wa upinzani Macky Sall.
Hawa Sow, mkazi wa Dakar anasema watu hawakulala usiku wa Jumapili kuamkia Jumatatu. “Hatujui lini matangazo rasmi yatakapotangazwa, lakini huu ni mshangao mkubwa kwetu lakini tunafurahia kwamba wade amempigia simu Sall kumpongeza ni ushindi mkubwa kwa demokrasia.”
No comments:
Post a Comment